Jumanne, 31 Januari 2017

ONLY ME NO ONE ELSE



THE MOMENT YOU FEEL LIKE THE WORLD IS FOR YOU ONLY AND NO ONE ELSE
Maisha ni kitu cha ajabu sana kiasi kwamba kila mtu huwa na namna yake ya kuyaelezea maisha kutokana na uelewa wake, mambo mbalimbali aliyopitia na baahdi ya watu aliowahi kuishi nao kwa wakati Fulani. Ila hufika wakati maana hiyo ya maisha ambayo alkikuwa nayo au alikuwa anaifahamu na kuamini kuwa ngio maana kamilili na hata kuona kuwa za wengine ni uongo au mbwembwe tu hubadilika na kuwa tofauti kabisa na mwanzo. Ila hufika wakati mtu huyo kuanza kujiuliza kuwa ilikuwaje mwanzo nikawa na maana ile na sasa hivi nina maana nyingine jibu huja ni kutokana na mazingira husika yanayomzunguka mtu huyo.
Ila ninachoamini mm ni kwamba maana nzuri na yenye ukweli katika maisha huja pale unapolkuwa katika wakati flani ambao hukuwaza kabla kama utakuja kuwa katika wakati kama huo. Nadhani utakuwa unajiuliza maswali mengi kwamba nn maana ya maneno haya ninayosema na kipi kinanifanya nipate uwezo wa kuongea maneno haya. Kamwe huwezi simulia vizuri maumivu ya kun’gatwa na nyoka kama hujawahi kun’gatwa na nyoka hata siku moja. Na ili ujue vizuri vizuri utamu wa mapenzi lazima uwe umeumizwa sehemu out of that it is difficult to realize the potentiality of a thing while you still with it. Simaanishi kuwa lazima kipotee kwanza ndo ujue bali lazima upate shida ya kile kitu ndo utajua vizuri. Mfano huwezi tambua umuhimu wa jembe kama haulimi au unalima ila sio kwa kwa kutumia jembe la mkono.
Kila binadamu hupitia mambo mbalimbali ambayo kwa upande mmoja humpa njia ya kujifunza mambo Fulani katika maisha ila kwa upande mwingine humfanya apoteze hata ule uwezo alionao katika ufanisi wa mambo kwani hujikuta kana kwamba anaelemewa sana na mambo yanayomzunguka na kuhisi kuwa dunia ni ya kwake peke yake. Mimi binafsi nakiri hilo kwani kwa kwa mambo ambayo yamenitokea katika mwaka huu wa 2016 kiasi flani sio rahisi kusema kwamba ni mambo ya kawaida bali mwisho wa siku tunasema inabidi umshukuru Mungu kwa kila jmbo kwani yy ndie mtoaji wa yote hapa duniani. Lakini bado unaweza kujiuliza kitu kuwa tunaamini na tunajua kuwa Mungu wetu ni muweza na ana upendo kwa wote ni kwann huwa anaruhusu masononeko kwa wana wake na kwann anruhusu mabaya yawapate wale anaowapenda?
Unaweza kuona watumishi wa Mungu wengi wanaofanya kazi yake kwa bidii na kikamilifu nao hufika wakati nao wanapatwa na magumu katika maisha je ni kwanini? Nabii isaya anatuambia kuwa ni vigumu sana kuzitambua njia za bwana kwani zipo juu sana na mawazo yake yapo juu sana hivyo sio rahisi kutambua maana ya mambo yanayotokea katika ulimwengu huu pasipo kumshirikisha roho mtakatifu. Mungu huwa na njia nyingi sana katika kuwaelekeza watu wake juu ya mambo ambayo wanapaswa kuyafanya duniani. Pale unaposogea hatua moja na mtu akakurudisha hatua mbili nyuma huwa ni changamoto sana hasa kwa maisha ya sasa hivi. Ukweli mwaka huu wa 2016 umekuwa mwaka wa changamoto sana kwangu kwani ukiachilia mbali kitendo cha kuibiwa pc siku ya jumapili nikiwa nipo kanisani unaweza kujiuliza inakuwaje unaenda kuabudu halafu Mungu anaruhusu mambo kama hayo kutokea. Lakini ikiwa hiyo haitoshi bado nimekuwa nikipata shida za hapa na pale kdili siku zinapoenda kuna wakati nimepata shida ya kutokuelewa ninachosoma hadi nikamfuata sister rosermistica kwa ajili ya ushauri.
Mnamo tarehe 02 december siku ya ijumaa nikiwa natoka misa ya asubuhi kanisani nilikuta ujumbe kwenye simu yangu ya kuwa bibi yangu wa moshi Mungu amemuita kutoka dunia hii. Nilihuzunika kama binadamu mwenye hisia na moyo wa nyama unavyoweza kupokea mambo. Nikiwa kwenye mipango ya kujiandaa kwa ajili ya kuondoka kusudi niweze kwenda kushiriki katika mazishi ya bibi hapo jumanne kama ilivyokuwa imepangwa nikapata tena taarifa ya kutokea kwa msiba wa babu upande wa mama. Nilipata kigugumizi ila nikayapokea yote kama mwanaume ambaye natakiwa kujikaza ili niweze kufanya mambo mengine. Nikafanikiwa kujiandaa na kusafiri siku ya jumatatu na kufika moshi kwa ajili ya kuhudhulia mazishi ya bibi. Lakini asubuh ya siku ya jumanne ambayo ndio siku ya mazishi yenyewe ndio nikapata tatizo jingine la kuibiwa simu yangu aina ya tecno c8. Ukweli kwa wakati ule niliona kama jambo la kawaida kwani bado nilikuwa na maumivu ya misiba yote miwili hivyo sikuona kama ni kitu cha kuniumiza sana kwa wakati huo.
Tulifanya juhudi za kuweza kuitafuta ili angalau kama inaweza kuonekana ila mpaka ninaondoka kule siku ya jumatano asubuh ilikuwa bado haijapatikana na juhudi ya kuitafuta ili kujua inaweza kuwa wapi bado zinaendelea na naamini Mungu zitazaa matunda kwa wakati unaompendza Mungu mwenyewe. Nilifanikiwa kufika kwamgwe salama na kuwakuta baadhi ya watu wameshaondoka ila waliokuwepo tulisalimiana na nikaenda kuona mahali babu alipopumzishwa pamoja na kusali . nikarudi na kuendelea na mambo mengine kabla ya kuondoka kesho yake kwa ajili ya kurudi chuoni kuendelea na majukumu ya kielimu kama tulivyochagua kuwa.
Lakini ukweli nimekuja kupata maumivu ya simu ile niliyoipoteza baada ya kutoka moshi na imenisumbua sana na kujikuta nikikumbuka mambo mengine mengi yaliyopita ikiwa ni pamoja na mtu ninatemdai kiasi cha pesa milioni moja na laki sita ambazo mpaka sasa sijajua kama atanilipa au la, na hayo yote yamekuwa ya  kiniongezea mawazo siku hadi siku. Sasa hapo ndo unaweza kuona kuwa mtu huyu unapomuuliza nn maana ya maisha atakupa jibu gani. Inafikiwa wakati hadi unapomuona mtu anacheka unajiuliza hivi huyu anacheka nn au kwann anacheka wakti mm mwenyewe nakitafuta kicheko hicho ila sijakipata bado. Unatamani kupata mtu wa kukufariji lakini unajikuta kuwa yupo mbali sana au hayupo kabisa so unakuwa katika wakati mgumu sana kimawazo na kifikra pia.
Ila kikubwa ni kumtegemea Mungu tu kwani ndiye mweza yote hapa duniani na kila wakati hutuombea mema na inawezekana hutupa haya ili atuepushe na mengine ambayo yangeweza kuwa mabaya sana kwetu na hata kwa wenzetu wanaotuzunguka. All in all we say thanks for everything because the one who give he knows us more than what we know him. Therefore as we faithful children of God we should be humble in praying so as our God may give us strength and courage of moving on without any worry on the way.
Njau martin R
Forest Voice {FV}
0717599375
GRORY BE TO GOD FOREVER AND EVER
AMEN

LOVE WHAT YOU GET



SOMETIME YOU HAVE TO LOVE WHEN YOU GET IT OR YOUR SURE OF GETTING IT”
“WAKATI MWINGINE INABIDI UPENDE BAADA YA KUPATA AU KUWA NA UHAKIKA WA KUPATA “
Ni matumaini yangu kuwa u mzima wa afya na unaendelea vizuri na shughuli za ujenzi wa taifa hili. Na kama utakuwa pia hufanyi hivyo basi utafanya kazi ya kusifia kuwa taifa limependeza au dunia imependeza japokuwa hujashiriki kuipendezesha ila kutokana tu labda na maombi yako basi tumefika hapo tutakapokuwa. Katika maisha hakuna mtu ambaye hana upndo wa dhati japokuwa hutokea wakati ukaingia doa kutokana na mabonde na milima ya hapa na pale ambayo katika maisha ni kitu cha kawaida. Wapo ambao walishasema na hata kujifanya wanaapa kuwa hawatapenda tena ila mwisho wa siku ndio wanakuwa wapendaji wazuriri sana watoto wa mjini tunasema unaingia baharini kwa miguu yote miwili hauna wasiwasi wa mamba wala kiboko kwakuwa unajihisi ni mamba ya ya mamba na kiboko zaidi ya kiboko. Kiukweli ni nzuri na inafurahisha lakini lazima uangalie nguvu ya kubadilisha moja kuwa saba na saba kuwa moja je ni sawa au ipi rahisi.
Hakuna kitu kizuri kama kupenda asikwambie mtu kwa kuwa unaweza hisi una uweza wa kupigana na simba dume  mwenye njaa bila silaha yoyote na ukamuua bila hat akupata jeraha lolote mwilini. Kwa uhalisia ni kama ndoto ila kiimani inawezekana kabisa tena ni kitu kdogo sana. Kama wote tungeweza kuwa na imani kama hizi za kupigana na simba na kumuua bila kupata jeraha lolote hakika ingekuwa vizuri sana ila kutokana na uhalisia na story tunazosikia juu ya ukali wa simba huwa tunajikoki sana na mwisho wa siku inakuwa tunavizia akitotea tu ndio tunafanya mambo na wakati mwigine woga wetu hutufanya kurudi na majeraha ambayo wakati mwingine hata hayatokani na simba labda kutokana na woga wetu ambao tumekuwa nao na kujikuta tukikwarza kwenye miti na hata kuanguka.
Ila ninachoamini mimi ni kwamba porini hayupo simba peke yake wapo wanyama wengi wapole na wanyenyekevu kama tembo twiga swala na wengine wengi ila tatizo letu tunapoenda tunahisi kukutana na simba tu na pia hatufikirii kuwa simba haishi kila sehemu ana maeneo yake maalum ya kuishi. Hivyo makosa yetu ni kufikiria kuwa porini wapo simbatu na hata pale anapotokea swala au hata sungura unatumia nguvu zilezile za kupambana na simba kupambana nae na hapo ndipo hupandikiza roho ya usimba juu ya viumbe hawa wadogo na baada ya hapo wanakuwa kama simba lakini kiuhalisia sio.
Hapa nataka kumaanisha kuwa hakuna mwanamke yeyote au mwanaume yeyote anayependa kuumizwa au kumuumiza mwenzake na kama ingekuwa hivyo mbona zamani watu walikuwa wanaanza urafiki ,uchumba ndoa mpaka wanazeeka pamoja bila shida yoyote. Ila kwa sasa utasikia ooh kaondoka kaenda kwao, mara hajalala ndani wiki moja ,mara hahudumii watoto n.k. Na bora hata mkifika huko mmejitahidi wengine maskini wanaishia kuitwa wapenzi tu hata hatua ya kuitwa mchumba bado na anatarajia kuzeeka ,na wengine wanaishia kuitwa wachumba tu unajiuliza hivi miaka hii ndoa hufungwa baada ya miaka kumi maana kila siku unatambulishwa tu ya kama kozi ya darasani kila mtu akipitia pale anafundishwa then akihama darasa haondoki nayo anaiacha hapohapo. Inasikitisha na inakatisha tamaa.
Lakini hebu tuangalie tatizo liko wapi na nin chanzo cha tatizo hilo? Kuna vitu viwili hapa ambavyo ningependa kuwashirikisha. Kimoja ni kwamba huwa tunapenda sana kwanza kabla hatujajua kuwa je tutafanikiwa au la.Sisemi kuanza kupenda kitu kabla hujakipata ni kosa naomba nieleweke hivi kuwa kupenda kitu sana kabla hujakipata au huna uhakika wa kukipata ni sumu. Utaniuliza sumu kivip? Sumu kwasababu wew utakuwa mipango yote na jitihada zako zote zitakuwa juu ya kitu hicho na mwisho wa siku unapokikosa nadhani unajua nn hutokea, wanaita mvulugano wa kifikra hivyo unachoona chochote mbele yako ili kuondoa machungu ya kukikosa kile cha mwanzo basi wew nacho then kama hukuwepo eneo la tukio. Ni imani yangu kuwa tupo pamoja katika mada hii najaribu kutumia lugha nyingine ila mantikia ya somo hili ni kuhusu swala zima la mapenzi kati ya mwanamke na mwanaume.
Kitu kingine ni kwamba kutokana na ile dhana tulionayo  kuwa porini wanakaa simba tu basi tunapoenda tunahisi kukutana na simba tu. Namaanisha tuna dhana ambayo haitufanyi tukaaminiana mwanamme anasena mwanamke hatuliagi hata siku moja na huku nako mwanamke anasema wanaume wote baba yao mmoja akimaanisha tabia zao zinafanan ambazo ni mbaya zote. Nahisi unaweza ukapata picha juu ya mechi hii ya mahasimu wawili inaishia kwa matokeo gani kwani kila mtu amejiandaa vya kutosha kupiga mshambulizi ya kufa mtu.
Sasa kibaya zaidi ni pale wanapokutana mwanamke ambaye hana hizo athari za mawazo hayo ila mwanamme aliye nae anazo hivyo baada ya mwanaume kula kona ndo mwanamke nae anashituka kwamba kumbe ndo kulivyo hivyo na yy anajipanga sasa unaweza ukaona hii chain itaishia wap. Sasa kipi cha kufanya?
Acha kumpenda sana kabla hujampata au huna uhakika wa kumpta kwani utakapomkosa utaumia sana na ndio chanzo cha mengine yote kutokea. Narudia tena simaanishi usimpende kwani mwanaume hawezi mfuata mwanamke kabla hajavutiwa nae na kumpenda na vivyohivyo mwanamke kwa mwanaume. Ila ninachoshauri mimi “USIMPENDE SANA UKAMFANYA KILA KITU KWAKO” wakati hujampata na wala huna uhakika wa kumpata otherwise utalazimisha uvunje uhusiano wao au wewe mwenyewe ufanye mambo ambayo hayapo.
Pia tuache mawazo ya kwamba kila mwanamke au mwanaume ni mhuni au sio mwaminifu kwenye mapenzi kwani tukifanya hivyo nani atabaki sasa cos wote tutakuwa at the samw pot hivyo hatutafika popote kwa hali hiyo. Tambua mapenzi ni matamu unapopendwa ila ni noma pale unapotendwa au usipopendwa wakati teari wewe ulishaweka malengo mengi juu ya mtu huyo.
“REMEMBER LOVE CAN MAKE U LIVE AND THE SAME LOVE CAN LET U GO BE CAREFUL “
NJAU MARTIN R
MTAALAM WA MITI
njaumartin@gmail.com
0717599375

PENZI LA MWANZO



PENZI LA MWANZO NI KAMA ARDHI AMBAYO HAIJAWAHI KUTUMIKA
Mwaka ndo unakamilika na tunatarajia kuanza mwaka mpya ambao waswahili wanasema mwaka mpya na mambo mapya. Msemo huu haumaanishi kuwa tuache kila kitu tulichokuwa tunafanya mwaka huu na tuanze vitu vipya hapana ila ni kuwa na mipango ile yenye mafanikio na kuongeza mingine ya kujiendeleza.
Thamini sana penzi lako la mwanzo kwani huwa ni la dhati na la kweli. Penzi hili hufanana na ardhi ambayo haijawahi kulimwa hata mara moja na pale inapoanza kulimwa mazao yake huwa ya kipekee sana tofauti na miaka yote itakayofuata. Moyo ni kiungo ambacho huwa hakipendi usumbufu sana ni sawa na mtoto mdogo unapomfundisha kitu hukishika sana tofauti na akiwa mkubwa. Moyo hupokea kwa dhati upendo ule ambao huja kwa mara ya kwanza na kujiaminisha kuwa ndio pekee na hakuna mwingine kama huo. Ila inapotokea upendo ule ukafa au kuondoka moyo huwa na wasiwasi na hapo ndipo akili huchukua jukumu la kufundisha moyo kupokea upendo tena na ikibidi kuulazimisha kupenda kitu ambacho ni hatari sana katika tasnia nzima ya mapenzi. Thamini penzi lako la mwanzo pia mthamini yule ambaye moyo umekubali kumpokea kwa mara ya kwanza wakati ukiwa pure. Kama tutajitahidi kuwa hivi basi maumivu katika mapenzi hayatakuwepo na itakuwa amani tu.
NOTE                                                                  
Kumbuka moyo haufundishwi kupenda wala kulazimishwa kupenda inapofikia hatua hiyo jua kuna tatizo sehemu na kuwa makini sana katika hilo kwani majuto anaweza kuwa jirani yako au ndugu yako kabisa.
EPUKA KUWA SABABU YA FULANI KUCHUKIA MAPENZI NA HATA NDOA KWANI NDOA NI AGIZO KUTOKA KWA MUNGU NAYO IHESHIMIWE NA KILA MTU
“WISH YOU HAPPY NEW YEAR 2017”
NJAU M
FOREST VOICE {PF}
0717  599375

WISH TO LIVE



WISH TO LIVE A CERTAIN LIFE BUT FOR THE PRESENT TIME LIFE AS YOU ARE
“DON’T LIVE THE LIFE BEFORE YOU GET INTO THAT LIFE”
In life there are many things of which someone may encounter when proceeding with the life journey. And from those things actually other things are so amazing of which need an extra attention and knowledge to withstand them. Everyone do wish to have a certain life or to live a certain life in his time here on earth. That is a very good thing of which everyone should dare to have it or even to lean from others. Everyone should think a certain life of which is better than what he/she have now.


But the problem comes on the  matter of making rehase of the life we would like to live before the actual life. That is what we call living the life before the life itself. The big issue here is not to wish to live a certain life but living it before which lead to denial of the life you have. Denying the life you have is simply denying yourself. What do I mean denying yourself… this means that you don’t value yourself and fill like God has mistaken you to put you in this world. Let take time, accept the life we have and prepare yourself for the life we wish to have. Don’t live the life of which you don’t have. Wait your time is coming of living that life.
“LIFE IS GOOD WHEN YOU ACCEPT WHO YOU ARE”
Njau M
MTAALAM WA MITI
njaumartin@gmail.com
0717599375