THE MOMENT YOU FEEL
LIKE THE WORLD IS FOR YOU ONLY AND NO ONE ELSE
Maisha ni kitu cha ajabu sana kiasi kwamba kila mtu
huwa na namna yake ya kuyaelezea maisha kutokana na uelewa wake, mambo
mbalimbali aliyopitia na baahdi ya watu aliowahi kuishi nao kwa wakati Fulani. Ila hufika wakati maana
hiyo ya maisha ambayo alkikuwa nayo au alikuwa anaifahamu na kuamini kuwa ngio
maana kamilili na hata kuona kuwa za wengine ni uongo au mbwembwe tu hubadilika
na kuwa tofauti kabisa na mwanzo. Ila hufika wakati mtu huyo kuanza kujiuliza
kuwa ilikuwaje mwanzo nikawa na maana ile na sasa hivi nina maana nyingine jibu
huja ni kutokana na mazingira husika yanayomzunguka mtu huyo.
Ila ninachoamini mm ni kwamba maana nzuri na yenye
ukweli katika maisha huja pale unapolkuwa katika wakati flani ambao hukuwaza
kabla kama utakuja kuwa katika wakati kama huo. Nadhani utakuwa unajiuliza
maswali mengi kwamba nn maana ya maneno haya ninayosema na kipi kinanifanya
nipate uwezo wa kuongea maneno haya. Kamwe huwezi simulia vizuri maumivu ya
kun’gatwa na nyoka kama hujawahi kun’gatwa na nyoka hata siku moja. Na ili ujue
vizuri vizuri utamu wa mapenzi lazima uwe umeumizwa sehemu out of that it is
difficult to realize the potentiality of a thing while you still with it.
Simaanishi kuwa lazima kipotee kwanza ndo ujue bali lazima upate shida ya kile
kitu ndo utajua vizuri. Mfano huwezi tambua umuhimu wa jembe kama haulimi au
unalima ila sio kwa kwa kutumia jembe la mkono.
Kila binadamu hupitia mambo mbalimbali ambayo kwa
upande mmoja humpa njia ya kujifunza mambo Fulani katika maisha ila kwa upande
mwingine humfanya apoteze hata ule uwezo alionao katika ufanisi wa mambo kwani
hujikuta kana kwamba anaelemewa sana na mambo yanayomzunguka na kuhisi kuwa
dunia ni ya kwake peke yake. Mimi binafsi nakiri hilo kwani kwa kwa mambo
ambayo yamenitokea katika mwaka huu wa 2016 kiasi flani sio rahisi kusema
kwamba ni mambo ya kawaida bali mwisho wa siku tunasema inabidi umshukuru Mungu
kwa kila jmbo kwani yy ndie mtoaji wa yote hapa duniani. Lakini bado unaweza
kujiuliza kitu kuwa tunaamini na tunajua kuwa Mungu wetu ni muweza na ana
upendo kwa wote ni kwann huwa anaruhusu masononeko kwa wana wake na kwann
anruhusu mabaya yawapate wale anaowapenda?
Unaweza kuona watumishi wa Mungu wengi wanaofanya
kazi yake kwa bidii na kikamilifu nao hufika wakati nao wanapatwa na magumu
katika maisha je ni kwanini? Nabii isaya anatuambia kuwa ni vigumu sana
kuzitambua njia za bwana kwani zipo juu sana na mawazo yake yapo juu sana hivyo
sio rahisi kutambua maana ya mambo yanayotokea katika ulimwengu huu pasipo
kumshirikisha roho mtakatifu. Mungu huwa na njia nyingi sana katika kuwaelekeza
watu wake juu ya mambo ambayo wanapaswa kuyafanya duniani. Pale unaposogea
hatua moja na mtu akakurudisha hatua mbili nyuma huwa ni changamoto sana hasa
kwa maisha ya sasa hivi. Ukweli mwaka huu wa 2016 umekuwa mwaka wa changamoto
sana kwangu kwani ukiachilia mbali kitendo cha kuibiwa pc siku ya jumapili
nikiwa nipo kanisani unaweza kujiuliza inakuwaje unaenda kuabudu halafu Mungu
anaruhusu mambo kama hayo kutokea. Lakini ikiwa hiyo haitoshi bado nimekuwa
nikipata shida za hapa na pale kdili siku zinapoenda kuna wakati nimepata shida
ya kutokuelewa ninachosoma hadi nikamfuata sister rosermistica kwa ajili ya
ushauri.
Mnamo tarehe 02 december siku ya ijumaa nikiwa
natoka misa ya asubuhi kanisani nilikuta ujumbe kwenye simu yangu ya kuwa bibi
yangu wa moshi Mungu amemuita kutoka dunia hii. Nilihuzunika kama binadamu
mwenye hisia na moyo wa nyama unavyoweza kupokea mambo. Nikiwa kwenye mipango ya
kujiandaa kwa ajili ya kuondoka kusudi niweze kwenda kushiriki katika mazishi
ya bibi hapo jumanne kama ilivyokuwa imepangwa nikapata tena taarifa ya kutokea
kwa msiba wa babu upande wa mama. Nilipata kigugumizi ila nikayapokea yote kama
mwanaume ambaye natakiwa kujikaza ili niweze kufanya mambo mengine.
Nikafanikiwa kujiandaa na kusafiri siku ya jumatatu na kufika moshi kwa ajili
ya kuhudhulia mazishi ya bibi. Lakini asubuh ya siku ya jumanne ambayo ndio
siku ya mazishi yenyewe ndio nikapata tatizo jingine la kuibiwa simu yangu aina
ya tecno c8. Ukweli kwa wakati ule niliona kama jambo la kawaida kwani bado
nilikuwa na maumivu ya misiba yote miwili hivyo sikuona kama ni kitu cha
kuniumiza sana kwa wakati huo.
Tulifanya juhudi za kuweza kuitafuta ili angalau
kama inaweza kuonekana ila mpaka ninaondoka kule siku ya jumatano asubuh
ilikuwa bado haijapatikana na juhudi ya kuitafuta ili kujua inaweza kuwa wapi
bado zinaendelea na naamini Mungu zitazaa matunda kwa wakati unaompendza Mungu
mwenyewe. Nilifanikiwa kufika kwamgwe salama na kuwakuta baadhi ya watu
wameshaondoka ila waliokuwepo tulisalimiana na nikaenda kuona mahali babu
alipopumzishwa pamoja na kusali . nikarudi na kuendelea na mambo mengine kabla
ya kuondoka kesho yake kwa ajili ya kurudi chuoni kuendelea na majukumu ya
kielimu kama tulivyochagua kuwa.
Lakini ukweli nimekuja kupata maumivu ya simu ile
niliyoipoteza baada ya kutoka moshi na imenisumbua sana na kujikuta nikikumbuka
mambo mengine mengi yaliyopita ikiwa ni pamoja na mtu ninatemdai kiasi cha pesa
milioni moja na laki sita ambazo mpaka sasa sijajua kama atanilipa au la, na
hayo yote yamekuwa ya kiniongezea
mawazo siku hadi siku. Sasa hapo ndo unaweza kuona kuwa mtu huyu unapomuuliza
nn maana ya maisha atakupa jibu gani. Inafikiwa wakati hadi unapomuona mtu
anacheka unajiuliza hivi huyu anacheka nn au kwann anacheka wakti mm mwenyewe
nakitafuta kicheko hicho ila sijakipata bado. Unatamani kupata mtu wa
kukufariji lakini unajikuta kuwa yupo mbali sana au hayupo kabisa so unakuwa
katika wakati mgumu sana kimawazo na kifikra pia.
Ila kikubwa ni kumtegemea Mungu tu kwani ndiye mweza
yote hapa duniani na kila wakati hutuombea mema na inawezekana hutupa haya ili
atuepushe na mengine ambayo yangeweza kuwa mabaya sana kwetu na hata kwa
wenzetu wanaotuzunguka. All in all we say thanks for everything because the one
who give he knows us more than what we know him. Therefore as we faithful
children of God we should be humble in praying so as our God may give us
strength and courage of moving on without any worry on the way.
Njau
martin R
Forest
Voice {FV}
0717599375
GRORY BE TO GOD FOREVER
AND EVER
AMEN