PENZI
LA MWANZO NI KAMA ARDHI AMBAYO HAIJAWAHI KUTUMIKA
Mwaka ndo
unakamilika na tunatarajia kuanza mwaka mpya ambao waswahili wanasema mwaka
mpya na mambo mapya. Msemo huu haumaanishi kuwa tuache kila kitu tulichokuwa
tunafanya mwaka huu na tuanze vitu vipya hapana ila ni kuwa na mipango ile
yenye mafanikio na kuongeza mingine ya kujiendeleza.
Thamini sana penzi
lako la mwanzo kwani huwa ni la dhati na la kweli. Penzi hili hufanana na ardhi
ambayo haijawahi kulimwa hata mara moja na pale inapoanza kulimwa mazao yake
huwa ya kipekee sana tofauti na miaka yote itakayofuata. Moyo ni kiungo ambacho
huwa hakipendi usumbufu sana ni sawa na mtoto mdogo unapomfundisha kitu
hukishika sana tofauti na akiwa mkubwa. Moyo hupokea kwa dhati upendo ule ambao
huja kwa mara ya kwanza na kujiaminisha kuwa ndio pekee na hakuna mwingine kama
huo. Ila inapotokea upendo ule ukafa au kuondoka moyo huwa na wasiwasi na hapo
ndipo akili huchukua jukumu la kufundisha moyo kupokea upendo tena na ikibidi
kuulazimisha kupenda kitu ambacho ni hatari sana katika tasnia nzima ya
mapenzi. Thamini penzi lako la mwanzo pia mthamini yule ambaye moyo umekubali
kumpokea kwa mara ya kwanza wakati ukiwa pure. Kama tutajitahidi kuwa hivi basi
maumivu katika mapenzi hayatakuwepo na itakuwa amani tu.
NOTE
Kumbuka moyo
haufundishwi kupenda wala kulazimishwa kupenda inapofikia hatua hiyo jua kuna
tatizo sehemu na kuwa makini sana katika hilo kwani majuto anaweza kuwa jirani
yako au ndugu yako kabisa.
EPUKA
KUWA SABABU YA FULANI KUCHUKIA MAPENZI NA HATA NDOA KWANI NDOA NI AGIZO KUTOKA
KWA MUNGU NAYO IHESHIMIWE NA KILA MTU
“WISH
YOU HAPPY NEW YEAR 2017”
NJAU
M
FOREST
VOICE {PF}
0717 599375
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni