“SOMETIME YOU HAVE TO LOVE WHEN YOU GET IT
OR YOUR SURE OF GETTING IT”
“WAKATI MWINGINE INABIDI UPENDE
BAADA YA KUPATA AU KUWA NA UHAKIKA WA KUPATA “
Ni matumaini yangu kuwa u mzima wa afya na unaendelea vizuri
na shughuli za ujenzi wa taifa hili. Na kama utakuwa pia hufanyi hivyo basi
utafanya kazi ya kusifia kuwa taifa limependeza au dunia imependeza japokuwa
hujashiriki kuipendezesha ila kutokana tu labda na maombi yako basi tumefika
hapo tutakapokuwa. Katika maisha hakuna mtu ambaye hana upndo wa dhati japokuwa
hutokea wakati ukaingia doa kutokana na mabonde na milima ya hapa na pale
ambayo katika maisha ni kitu cha kawaida. Wapo ambao walishasema na hata
kujifanya wanaapa kuwa hawatapenda tena ila mwisho wa siku ndio wanakuwa
wapendaji wazuriri sana watoto wa mjini tunasema unaingia baharini kwa miguu
yote miwili hauna wasiwasi wa mamba wala kiboko kwakuwa unajihisi ni mamba ya
ya mamba na kiboko zaidi ya kiboko. Kiukweli ni nzuri na inafurahisha lakini
lazima uangalie nguvu ya kubadilisha moja kuwa saba na saba kuwa moja je ni
sawa au ipi rahisi.
Hakuna kitu kizuri kama kupenda asikwambie mtu kwa kuwa unaweza hisi una
uweza wa kupigana na simba dume mwenye
njaa bila silaha yoyote na ukamuua bila hat akupata jeraha lolote mwilini. Kwa
uhalisia ni kama ndoto ila kiimani inawezekana kabisa tena ni kitu kdogo sana.
Kama wote tungeweza kuwa na imani kama hizi za kupigana na simba na kumuua bila
kupata jeraha lolote hakika ingekuwa vizuri sana ila kutokana na uhalisia na
story tunazosikia juu ya ukali wa simba huwa tunajikoki sana na mwisho wa siku
inakuwa tunavizia akitotea tu ndio tunafanya mambo na wakati mwigine woga wetu
hutufanya kurudi na majeraha ambayo wakati mwingine hata hayatokani na simba
labda kutokana na woga wetu ambao tumekuwa nao na kujikuta tukikwarza kwenye
miti na hata kuanguka.
Ila ninachoamini mimi ni kwamba porini hayupo simba peke yake wapo wanyama
wengi wapole na wanyenyekevu kama tembo twiga swala na wengine wengi ila tatizo
letu tunapoenda tunahisi kukutana na simba tu na pia hatufikirii kuwa simba
haishi kila sehemu ana maeneo yake maalum ya kuishi. Hivyo makosa yetu ni
kufikiria kuwa porini wapo simbatu na hata pale anapotokea swala au hata
sungura unatumia nguvu zilezile za kupambana na simba kupambana nae na hapo
ndipo hupandikiza roho ya usimba juu ya viumbe hawa wadogo na baada ya hapo
wanakuwa kama simba lakini kiuhalisia sio.
Hapa nataka kumaanisha kuwa hakuna mwanamke yeyote au mwanaume yeyote
anayependa kuumizwa au kumuumiza mwenzake na kama ingekuwa hivyo mbona zamani
watu walikuwa wanaanza urafiki ,uchumba ndoa mpaka wanazeeka pamoja bila shida
yoyote. Ila kwa sasa utasikia ooh kaondoka kaenda kwao, mara hajalala ndani
wiki moja ,mara hahudumii watoto n.k. Na bora hata mkifika huko mmejitahidi
wengine maskini wanaishia kuitwa wapenzi tu hata hatua ya kuitwa mchumba bado
na anatarajia kuzeeka ,na wengine wanaishia kuitwa wachumba tu unajiuliza hivi
miaka hii ndoa hufungwa baada ya miaka kumi maana kila siku unatambulishwa tu
ya kama kozi ya darasani kila mtu akipitia pale anafundishwa then akihama
darasa haondoki nayo anaiacha hapohapo. Inasikitisha na inakatisha tamaa.
Lakini hebu tuangalie tatizo liko wapi na nin chanzo cha tatizo hilo? Kuna
vitu viwili hapa ambavyo ningependa kuwashirikisha. Kimoja ni kwamba huwa
tunapenda sana kwanza kabla hatujajua kuwa je tutafanikiwa au la.Sisemi kuanza
kupenda kitu kabla hujakipata ni kosa naomba nieleweke hivi kuwa kupenda kitu
sana kabla hujakipata au huna uhakika wa kukipata ni sumu. Utaniuliza sumu
kivip? Sumu kwasababu wew utakuwa mipango yote na jitihada zako zote zitakuwa
juu ya kitu hicho na mwisho wa siku unapokikosa nadhani unajua nn hutokea,
wanaita mvulugano wa kifikra hivyo unachoona chochote mbele yako ili kuondoa
machungu ya kukikosa kile cha mwanzo basi wew nacho then kama hukuwepo eneo la
tukio. Ni imani yangu kuwa tupo pamoja katika mada hii najaribu kutumia lugha
nyingine ila mantikia ya somo hili ni kuhusu swala zima la mapenzi kati ya
mwanamke na mwanaume.
Kitu kingine ni kwamba kutokana na ile dhana tulionayo kuwa porini wanakaa simba tu basi tunapoenda
tunahisi kukutana na simba tu. Namaanisha tuna dhana ambayo haitufanyi
tukaaminiana mwanamme anasena mwanamke hatuliagi hata siku moja na huku nako
mwanamke anasema wanaume wote baba yao mmoja akimaanisha tabia zao zinafanan
ambazo ni mbaya zote. Nahisi unaweza ukapata picha juu ya mechi hii ya mahasimu
wawili inaishia kwa matokeo gani kwani kila mtu amejiandaa vya kutosha kupiga
mshambulizi ya kufa mtu.
Sasa kibaya zaidi ni pale wanapokutana mwanamke ambaye hana hizo athari za
mawazo hayo ila mwanamme aliye nae anazo hivyo baada ya mwanaume kula kona ndo
mwanamke nae anashituka kwamba kumbe ndo kulivyo hivyo na yy anajipanga sasa
unaweza ukaona hii chain itaishia wap. Sasa kipi cha kufanya?
Acha kumpenda sana kabla hujampata au huna uhakika wa kumpta kwani
utakapomkosa utaumia sana na ndio chanzo cha mengine yote kutokea. Narudia tena
simaanishi usimpende kwani mwanaume hawezi mfuata mwanamke kabla hajavutiwa nae
na kumpenda na vivyohivyo mwanamke kwa mwanaume. Ila ninachoshauri mimi
“USIMPENDE SANA UKAMFANYA KILA KITU KWAKO” wakati hujampata na wala huna
uhakika wa kumpata otherwise utalazimisha uvunje uhusiano wao au wewe mwenyewe
ufanye mambo ambayo hayapo.
Pia tuache mawazo ya kwamba kila mwanamke au mwanaume ni mhuni au sio
mwaminifu kwenye mapenzi kwani tukifanya hivyo nani atabaki sasa cos wote
tutakuwa at the samw pot hivyo hatutafika popote kwa hali hiyo. Tambua mapenzi
ni matamu unapopendwa ila ni noma pale unapotendwa au usipopendwa wakati teari
wewe ulishaweka malengo mengi juu ya mtu huyo.
“REMEMBER
LOVE CAN MAKE U LIVE AND THE SAME LOVE CAN LET U GO BE CAREFUL “
NJAU MARTIN R
MTAALAM WA MITI
njaumartin@gmail.com
0717599375
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni