Leo ni siku ya Misitu duniani, na hakuna mtu ambaye hajui umuhimu wa misitu popote pale alipo ikiwa ni kwa kusoma kwenye vitabu, kuambiwa au pia kujionea mwenyewe. Ujumbe wa mwaka huu ni "MISITU NA NISHATI". Ukweli ni kuwa karibia asilimia 80% ya nishati inatokana na misitu hivyo tunatakiwa kujua namna ya kutumia nishati hiyo kwa matumizi endelevu kwani tutakapoitumia vibaya ipo siku tutaikosa na itakuwa shida sana. Tuungane pamoja kulinda na kutunza misitu yetu kwa maendeleo endelevu, tuache tamaa ambazo zitatuletea majonzi baadae
Twende sambamba katika kampeni ya kutokomeza mabadiliko ya tabia nchi na athari zake tusiwaachie tu wataalam wa fani kwani sote tuna uwezo wa kufanya jambo kila mtu kwa nafasi yake. Kila mtu ajipongeze kwa kuwa mtuzaji mzuri wa misitu na sio kujisifu kwa kuwa mharibifu mbaya wa misitu. "TANZANIA BILA ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIA NCHI INAWEZEKANA, TUANZE MIMI NA WEWE HALAFU YULE NA WALE" By Njau M au Mtaalam wa Miti "Happy world forests day"
Jumanne, 21 Machi 2017
HAPPY WORLD FORESTS DAY.
Jumapili, 19 Machi 2017
YATUNZE NAYO YATAKUTUNZA
Uzuri wa mazingira yetu huletwa na utunzaji mzuri wa mazingira hayohayo yanayotuzunguka. Na katika kufanya maendeleo lazima tuwe yakinifu katika kujua faida za maendeleo hayo tutakapochagua maeneo sahihi na pia tunapochagua maeneo ambayo sio sahihi pia kuna athari kubwa tu kwetu na kizazi kijacho. Mfano Unapofyeka msitu kwa ajili ya kilimo ni kweli unahitaji kufanya jambo la kimaendeleo ila njia unayotumia au eneo ulilochagua sio sahihi. Kwani utaandaa shamba lako ila kumbuka unategemea mvua ili upate mazao sasa kutokana na uharibifu ulioufanya mvua inakosekana, je umefanya maendeleo au umejirudisha nyuma tena kibaya bora ingekuwa wewe pekeyako ila umerudisha nyuma hata wale wasio na hatia kwani kila mtu atakosa kupata mazao. Hivyo basi tufanye mambo ya kimaendeleo ikienda sambamba na kuheshimu mazingira yetu ili nayo yatutunze. "TANZANIA WITHOUT CLIMATE CHANGE EFFECTS IS POSSIBLE, IT BEGINS WITH ME AND YOU" By Mtaalam wa Miti. Follow me kupitia blog yangu ujifunze zaidi "njaumartin. blogspot. com"
Ijumaa, 17 Machi 2017
THINK GREEN ALWAYS IT PAYS
Tunateseka na kupata madhara kwa vitu ambavyo hatujafanya sisi. Athari za mabadiliko ya tabia nchi kila mtu anazifahamu ila chanzo chake kikubwa ni ongezeko la hewa ukaa (Green house gasses) ambazo hutokana na hewa chafu ya viwandani ambayo kiukweli kwa Tanzania au Afrika kwa ujumla kama ni kuchangia basi ni asilimia ndogo sana. Ila kama baba alikuwa masikini kwa kutokufanya kazi au kuwa na matumizi mabaya ya hela mtoto hutakiwi kila siku kulalamika kuhusu baba yako ila inatakiwa ujipange na maisha yako ujue yataendaje kwani teari ya kwake yameenda mpaka akafikia umri huo. Hivyo basi ni jukumu letu sote kuona kuwa tunapambana na hizi athari kwa njia ambazo zinaweza kutukomboa kama vile kupanda miti kwa bidii sana, kuepuka kukata miti ya asili kwani ina msaada mkubwa katika kupunguza hewa ukaa, kulinda vyanzo vyetu vya maji kwa kutolima katika vyanzo vya maji, kuelimishana juu ya athari hizi kwa vizazi vijavyo na kikubwa kulinda na kutunza misitu iliyopo kwa maendeleo endelevu. Kwa pamoja tunaweza tuamke tuanze kazi. Athari za mabadiliko ya tabia nchi zinaweza kupunguzwa na kuondolewa kabisa. Tambua "FORESTS CONSERVATION IS THE SOLUTION FOR CLIMATE CHANGE" By Mtaalam wa Miti.
FAIDIKA BILA KULETA ATHARI
Hii ni faida ambayo hutokana na uvunaji wa miti ambayo hutupatia hela nyingi. Lakini faida hii huwa kilio endapo tunaipata kutoka katika misitu ya asili ambayo haitakiwi kuvunwa kwani kwa kufanya hivyo tunazidi kuongeza athari za mabadiliko ya tabia nchi. Hivyo faida hupatikana kwa kupanda miti sisi wenyewe na kwa sasa wataalam wametuwezesha kuweza kupata mazao haya kwa muda mfupi tofauti na mwanzo unapanda anakuja kuvuna mtoto wako kwa sasa unapanda mwenyewe na unavuna ukiwa bado una nguvu. Tushirikiane kutokomeza uvunaji wa miti katika misitu ya asili hebu tupande miti ili tupate faida na kujikinga na mabadiliko ya tabia nchi. Tuache ukatili kwani mimi na wewe tutapata hela leo lakini itakuwa kilio cha mda mrefu kwa watoto wetu. Tuwapende na kuwathamini kizazi kijacho. Ungana nami kwa kusambaza ujumbue huu pia like na comment kuongeza ufanisi. TANZANIA WITHOUT CLIMATE CHANGE EFFECTS IS POSSIBLE, IT BEGINS WITH ME AND YOU" By Mtaalam wa Miti
Jumapili, 5 Machi 2017
USIFANYE JAMBO KWA KUWA KUNA KUFANYA.....
njau martin
njaumartin@gmail.com
0717599375