Ijumaa, 17 Machi 2017

FAIDIKA BILA KULETA ATHARI

Hii ni faida ambayo hutokana na uvunaji wa miti ambayo hutupatia hela nyingi.  Lakini faida hii huwa kilio endapo tunaipata kutoka katika misitu ya asili ambayo haitakiwi kuvunwa kwani kwa kufanya hivyo tunazidi kuongeza athari za mabadiliko ya tabia nchi.  Hivyo faida hupatikana kwa kupanda miti sisi wenyewe na kwa sasa wataalam wametuwezesha kuweza kupata mazao haya kwa muda mfupi tofauti na mwanzo unapanda anakuja kuvuna mtoto wako kwa sasa unapanda mwenyewe na unavuna ukiwa bado una nguvu.  Tushirikiane kutokomeza uvunaji wa miti katika misitu ya asili hebu tupande miti ili tupate faida na kujikinga na mabadiliko ya tabia nchi. Tuache ukatili kwani mimi na wewe tutapata hela leo lakini itakuwa kilio cha mda mrefu kwa watoto wetu. Tuwapende na kuwathamini kizazi kijacho.  Ungana nami kwa kusambaza ujumbue huu pia like na comment kuongeza ufanisi.  TANZANIA WITHOUT CLIMATE CHANGE EFFECTS IS POSSIBLE, IT BEGINS WITH ME AND YOU" By Mtaalam wa Miti

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni