Jumapili, 5 Machi 2017

ISHI KUTOKANA NA JAMII ILA USITENDE DHAMBI



“ISHI KUTOKANA NA MAZINGIRA LAKINI USITENDE DHAMBI”

“LIVE ACCORDING TO THE ENVIRONMENT BUT DO NOT SIN”

Habari siku ya leo mpendwa wangu ,ni matumaini yangu kuwa u mzima na unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku. Napenda kumshukuru mungu kwa kutulinda na hatari zote na kutufikisha hapa tulipo, kwani ni wengi walipenda kufika ila hawakuweza ila kwa sisi tuliofanikiwa kufika basi tutambue kuwa si kwa uwezo wetu bali ni kwa uwezo wa yule aliyetuumba.

Karibuni tena katika safu yetu ya kushirikishana vitu mbalimbali vinavyohusu mambo mbalimbali ya kijamii na jinsi ya kuishi kwa furaha na amani na jamii inayotuzunguka. Leo napenda tushirikishane kitu kimoja ambacho ni “kuishi kutokana na mazingira au jamii lakini usitende dhambi”

Watu wengi husema kuwa maisha ni kwa ajili yangu na hivyo kila ninachokifanya kinakuwa na implication kwangu tu na sio kwa mtu mwingine. Hiyo sio sawa na naomba tuifute hiyo dhana katika vichwa vyetu kwani inapoteza kabisa. Ukweli maisha sio yako peke yako bali maisha unatakiwa uishi kwa ajili ya wengine. Kwa wale wakristu tunaamini kuwa mwanadamu wa kwanza kuumbwa alikuwa adam na huyo Mungu alimuumba kutoka kwenye udongo. Ila Mungu mwenyewe akaona sio vyema kwa adamu kuwa peke yake akamfanyia msaidizi wa kufanana nae, hebu fikiria kama ungekuwa pekeyako katika dunia hii ingekuwaje, nikiwa na maana ya kwamba hakuna wazazi wala walezi wala mtu yeyote yule , nadhani maisha yangekuwa magumu sana kwani upweke ungetawala sana hivyo kumbe Mungu hakukosea kumfanyia adamu msaidizi wa kufanana nae.

Inashangaza sana mtu anakuambia kuwa Mungu anaangalia moyo tu ,kama ni hivyo mbona Mungu aliwafanyia nguo za magome ya miti adamu na hawa walipoasi unahisi alikuwa anaonesha nn? Labda unahisi alikosa kazi ila sivyo alikuwa na maana kuwa japokuwa yeye anaangalia moyo lakini moyo upo ndani ya nn?
 Na je kuna uhusiano gani kati ya moyo na mwili? Tuangalie mke wa ruthu aligeuka jiwe la chumvi , swali ni kwann haukugeuka moyo tu jiwe la chunvi ukageuka mwili mzima? Pia katika hali ya kawaida tunaona kuwa pale moyo unapoumia viungo vyote vya mwili huweza kupata ile athari iliyokuwapo kwenye moyo je ushawahi kujiuliza ni kwanini inakuwa hivyo?
 Ukweli ni kwamba ukatae usikubali upo uhusiano mkubwa sana kati ya moyo na mwili. Na katu moyo hauwezi kuwepo bila mwili vivyo hivyo mwili bila moyo.

Ukiangalia kwa makini utaona kuwa tunatakiwa tuishi pasipo kuwa vikwazo kwa watu wengine. Unaweza kuwa kikwazo kwa watu wengine either kwa kujua au kwa kutokujua ndo maana nikaita somo hili ni kuishi kutokana na jamii husika au mazingira husika lakini usitende dhambi. 
 Papa fransis amewahi kusema “life lived without others is not a life” Unapomkwaza mwenzako na kumpelekea either kutenda dhambi au kumsogeza karibu na mazingira ya kutenda dhambi basi nadhani adhabu yako unaijua ya kwamba ni bora ufungiwe jiwe la kusagia shingoni na ukatupwe baharini sio maneno yangu bali ni maandiko matakatifu ndio yanatuelekeza hivyo. Sasa ndugu yangu acha dhana ya kwamba hata nikivaa vibaya , nikitukana sana ,nikilewa sana ili mradi simfanyii mtu direct ikiwa na maana kumtukana mtu au kunywa pombe kwa ajili ya mtu au kuvaa vibaya kwakuwa tu umependa eti kwa kuwa Mungu haangalii ya nje umepotea kumbuka unachofanya ndio kinachokuonesha jinsi ulivyo ndani mwako hivyo tuwe makini na vitu ambavyo tunavifanya kwa kuwa hututambulisha kwa watu wengine bila sisi wenyewe kujua.

Inatupasa tutambue kuwa ile amri ya kwamba mpende jirani yako kama nafsi yako ina upana sana na haiishii tu katika kusaidiana ki material things ila hata kiroho ndio zaidi. Hapa namaanisha unapofanya mwenzio akafa kiroho ujue una kitu cha kujibu kwani hapo hakuna upendo tena bali ni chuki na kutaka mwenzako nae aende motoni kama ww ulivyochagua. Samahani usije ukanikariri vibaya kwamba ninakuhukumu la hasha unajihukumu mwenyewe kwa matendo yako. Mimi wajibu wangu ni kukumbusha tu nn unatakiwa kufanya.

Tunapoambiwa tuwapende jirani zetu kama tunavyojipenda wenyewe ina maanisha kuwa tuwasaidie pia kutoingia majaribuni na kuwaokoa pale wanapoingia kwa bahati mbaya ila sio kufurahia kuwa ngoja tumuone alikuwa anaringa sana sasa amepatikana hapana hatupaswi kuishi hivyo. Na ndio maana tuna jukumu la kuishi kwa ajili ya wenzetu na sio sisi peke etu kwani kwa maisha hayo hayatatusaidia kufika kule ambako Mungu ametuandalia tufike.

Hakika tukiishi kwa ushirikiano tutaweza kutimiza yale ambayo Mungu ametuelekeza tufanye na hakika tutaishi kwa amani sana huku kila mmoja akiwa na ari ya kumtumikia Mungu kwa nguvu zote na kuikimbilia ile ahadi tuliyoahiwa naye Mungu wetu. Mwenyezi Mungu atubariki sote na kutuangazia uso wake na baraka zake zikawe nasi daima.

“BE BRAVE MORE THAN SNAKE BUT HAMBLE AS DOVE”

Njau martin

Mtaalam wa miti.

0717599375

Njaumartin48@gmail.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni