Jumapili, 5 Machi 2017

USIFANYE JAMBO KWA KUWA KUNA KUFANYA.....



“USIZAE WATOTO KWA KUWA KUNA KUZAA, ILA ZAA KWA KUWA UMEANDAA MAZINGIRA YA KUPOKEA MTOTO”
“DON’T HAVE A CHILD COS WE HAVE BEEN TOLD TO HAVE THEM, BUT HAVE A CHILD YOU ARE ABLE TO CARE HIM/HER”
Ni ukweli usiopingika kuwa upo wakati unafanya vitu ambavyo kwa hali ya kawaida sio kwamba umefikiria kwa makini ni kwanini unafanya hilo jambo ila labda ni kutokana na mazoea au kutokana na tamaduni za jamii fulani au pia kutokana na nani amefanya nini. Hii hutupelekea kufika sehemu na kujikuta tukisababisha maumivu kwa wengine either indirect or direct kwa kuwa wale ambao wanakuwa assosiated na hivi vitu huwa wanapata shida eneo fulani na kujikuta wanaathilika bila kuwa na hatia.  
Ninachotaka kusema hapa ni kwamba unapofanya kitu chochote hakikisha ya kwamba umeshaweka mazingira thabiti ya kuonesha kweli kile unachofanya umekitafakari na hujakurupuka kukifanya tu. Hii itakusaidia kuepusha baadhi ya mambo ambayo hayana ulazima kujitokeza na kuathili watu na mfumo wa maisha. Mfano suala la kupata watoto ni jambo zuri ila ni lazima ufikirie kwanza ni kwanini unataka kupata mtoto na je umemuandalia mazingira ya kuja kukaa kwa raha?
Yeye anapokuja hajui chochote kuhusu duniani na anatarajia kuja kuiona dunia nzuri na tamu ,ila pale inapotokea tofauti huwa kwake ni shida kwa kuwa hakutegemea hilo. Kama ww ulisoma kwa shida basi haimaanishi na mtoto wako nae asome kwa shida hivyohivyo ila inatakiwa basi umuandaliea mazingira ambayo yanaweza kumfanya awe na furaha na asione kama duniani ni sehemu mbaya kwake basi sehemu nzuri na yenye amani tele.
Nakazia sana katika suala la kupata mtoto kwa kuwa ndio sualal ambalo wengi huwa wanakosea na kujikuta wanajilaumu baadae kuwa ni kwanini walifanya hivyo. Haina haja ya kujilaumu baada ya muda ila kinachotakiwa kuwepo ni kuwa makini kuanzia mwanzo ili kuepuka matatizo ambayo yanaweza kujitokeza kwa namna yoyote ile labda itokee bahati mbaya sana. Usilete dhana ya kwamba kwakuwa mm nimesoma kwa vidumu so hata mwanangu anatakiwa asome kwa vidumu,  hatuishi kwa mazoea basi tunatakiwa tuishi kutokana na mazingira husika yalivyo.
Ila sio jambo hilo yapo mengi ambayo hatuna budi kuyaangalia ili kuweza kuweka mambo sawasawa. Hivyo kikubwa katika maisha ni bora uwe na moja uliyo na uwezo nayo kuliko kuwa na kumi ambazo huna uwezo nazo. Logic behind ni kwamba ridhika na unachokipata kwa muda husika na muombe Mungu akujalie zaidi kwa wakati wake kwani yeye ndo hujua wakati uliosahihi kwetu na wakati usio sahihi kwetu kwa ajili ya kutupa neema zake.
“ALWAYS BE GOOD TO THE PRESENT AND THE FUTURE"
njau martin
njaumartin@gmail.com
0717599375

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni