“USIZAE WATOTO KWA KUWA KUNA KUZAA, ILA ZAA KWA KUWA
UMEANDAA MAZINGIRA YA KUPOKEA MTOTO”
“DON’T HAVE A CHILD COS WE HAVE BEEN TOLD TO HAVE
THEM, BUT HAVE A CHILD YOU ARE ABLE TO CARE HIM/HER”
Ni ukweli
usiopingika kuwa upo wakati unafanya vitu ambavyo kwa hali ya kawaida sio
kwamba umefikiria kwa makini ni kwanini unafanya hilo jambo ila labda ni
kutokana na mazoea au kutokana na tamaduni za jamii fulani au pia kutokana na
nani amefanya nini. Hii hutupelekea kufika sehemu na kujikuta tukisababisha
maumivu kwa wengine either indirect or direct kwa kuwa wale ambao wanakuwa
assosiated na hivi vitu huwa wanapata shida eneo fulani na kujikuta wanaathilika
bila kuwa na hatia.
Ninachotaka
kusema hapa ni kwamba unapofanya kitu chochote hakikisha ya kwamba umeshaweka
mazingira thabiti ya kuonesha kweli kile unachofanya umekitafakari na
hujakurupuka kukifanya tu. Hii itakusaidia kuepusha baadhi ya mambo ambayo
hayana ulazima kujitokeza na kuathili watu na mfumo wa maisha. Mfano suala la
kupata watoto ni jambo zuri ila ni lazima ufikirie kwanza ni kwanini unataka
kupata mtoto na je umemuandalia mazingira ya kuja kukaa kwa raha?
Yeye anapokuja
hajui chochote kuhusu duniani na anatarajia kuja kuiona dunia nzuri na tamu
,ila pale inapotokea tofauti huwa kwake ni shida kwa kuwa hakutegemea hilo.
Kama ww ulisoma kwa shida basi haimaanishi na mtoto wako nae asome kwa shida
hivyohivyo ila inatakiwa basi umuandaliea mazingira ambayo yanaweza kumfanya
awe na furaha na asione kama duniani ni sehemu mbaya kwake basi sehemu nzuri na
yenye amani tele.
Nakazia sana
katika suala la kupata mtoto kwa kuwa ndio sualal ambalo wengi huwa wanakosea
na kujikuta wanajilaumu baadae kuwa ni kwanini walifanya hivyo. Haina haja ya
kujilaumu baada ya muda ila kinachotakiwa kuwepo ni kuwa makini kuanzia mwanzo
ili kuepuka matatizo ambayo yanaweza kujitokeza kwa namna yoyote ile labda
itokee bahati mbaya sana. Usilete dhana ya kwamba kwakuwa mm nimesoma kwa
vidumu so hata mwanangu anatakiwa asome kwa vidumu, hatuishi kwa mazoea basi tunatakiwa tuishi
kutokana na mazingira husika yalivyo.
Ila sio jambo
hilo yapo mengi ambayo hatuna budi kuyaangalia ili kuweza kuweka mambo
sawasawa. Hivyo kikubwa katika maisha ni bora uwe na moja uliyo na uwezo nayo
kuliko kuwa na kumi ambazo huna uwezo nazo. Logic behind ni kwamba ridhika na
unachokipata kwa muda husika na muombe Mungu akujalie zaidi kwa wakati wake
kwani yeye ndo hujua wakati uliosahihi kwetu na wakati usio sahihi kwetu kwa
ajili ya kutupa neema zake.
“ALWAYS BE GOOD TO THE PRESENT AND THE FUTURE"njau martin
njaumartin@gmail.com
0717599375
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni